MKAZI wa kijiji cha Lyapinda tarafa ya Wampembe wilayani Nkasi mkoani Rukwa Derick simfukwe (25) amehukumiwa kwenda jela miezi 12 au kulipa faini ya Tsh LAKI 5 na mahakamama ya wilaya Nkasi kwa kosa la kukutwa na Nyara za serikali.
Mtuhumiwa amekiri kutenda kosa hilo mbele ya Mahakama huku akiiomba mahakama hiyo isimpatie adhabu yoyote kwa maana hakujua kuwa mnyama huyo aina ya Insha ni nyara ya serikali.
Akitoa hukumu hiyo Hakimu mkazi wa mahakama hiyo Ramadhani Rugemalila ,amesema mtuhumiwa amekutwa na hatia baada ya kutenda kosa hilo .
Awali upande wa mashitaka ukiongozwa na mwendesha mashitaka wa jeshi la Polisi Hamimu Gwelo uliitaka mahakama kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa ili iwe ni fundisho kwa watu wengine wenye nia ya kutaka kutenda kosa kama hilo.
EmoticonEmoticon