SAMATTA AWAFARIJI WAKAZI WA BUKOBA WALIOKUMBWA NA TETEMEKO LA ARDHI


Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta anayecheza soka la kulipwa kwenye klabu ya Genk, Ubelgiji na kiungo wa kimataifa wa timu ya taifa ya Kenya na Tottenham ya Englnd, kwa pamoja wametuma salam za pole kwa wakazi wa Bukoba kutokana na janga la tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni.

Wawili hao kwa nyakati tofauti kila mmoja ameandika ujumbe wa salam za pole kwa wakazi wa Bukoba waliopoteza ndugu jamaa na marafiki pamoja na hasara ya mali baada ya kukumbwa na tetemeko la ardhi.

“Poleni wakazi wa Bukoba kwa kupoteza ndugu pamoja na mali kutokana na tetemeko la ardhi, Mungu awatie nguvu na pia tuwaombee waliotangulia”, unasomeka ujumbe wa Samatta kwenye account yake ya twitter.


EmoticonEmoticon