MACHAKU KUPELEKWA KWA MKOPO KLABU YOYOTE NCHINI KUJIREKEBISHA TABIA

 
KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Salum Machaku huenda  akatolewa kwa mkopo kwa nusu msimu kwa klabu yoyote kwenda kujifunza adabu kabla ya kurudishwa Wekundu wa Msimbazi.
 
Habari ambazo zimepatikana kutoka ndani ya Simba, zimesema kwamba Machaku amekuwa akijisikia mno baada ya kufanya vizuri msimu huu akiwa na jezi ya Wekundu wa Msimbazi kiasi cha kudharau  hata viongozi wa timu hiyo.
 
Naye kiongozi mmoja wa juu wa timu hiyo, amesema kwamba uongozi ulifanya jitihada kubwa za kumbadili kitabia Machaku, ikiwemo kumuweka chini ya mchezaji anayeogopwa na wachezaji wote, Haruna Moshi ‘Boban’, lakini ikashindikana.
 
Kwa tetesi zilizopo,Salum Machaku ni kati ya wachezaji ambao wamo kwenye orodha ya nyota wanaotakiwa na mahasimu wa jadi wa Simba,Yanga na katika siku za hivi karibuni, Machaku amekuwa karibu mno na kipa wa Yanga, Shaaban Hassan Kado ambaye waliwahi kucheza naye pamoja Mtibwa Sugar na timu ya taifa.


EmoticonEmoticon