KAMPUNI YA ARUSHA ART LIMITED YAZINDUA MAGARI MAPYA AINA YA VOLKSWAGEN AMAROK PICKUP

Kampuni ya Arusha Art Limited wakala wa kuuza magari aina Mercedes-Benz, Nissan na Suzuki kanda ya Kaskazini kwa kushirikiana na kampuni ya uuzaji na usambazaji wa magari mapya ya Alliance Autos Tanzania Ltd ya Tanzania imezindua gari mpya aina ya Volkswagen Amarok pickup katika viwanja vya Magereza katika maonyesho ya Karibu Travel and Tourism Fair yanayoendelea jijini Arusha.

Akiongea na Waandishi wa habari uwanjani hapo wakati wa uzinduzi wa gari hilo Meneja Biashara wa kampuni Alliance Autos Tanzania Ltd Tanzania ya kutoka jijini Dar es Salaam Alfred Minja alisema gari hilo ni imara kwa matumizi ya barabara za nchini Tanzania na Afika Mashariki.

Minja alidokeza kuwa gari hilo limetengenezwa kutoka nchini Ujerumani na ni mara ya kwanza kwa gari hilo kufika nchini na kuzinduliwa jijini Arusha kwa mara ya kwanza ingawa litazinduliwa jijini Dar es Salaam mwezi ujao.

“Gari hili Volkswagen Amarok pickup ni madhubuti kwa barabara za Tanzania na limetengenezwa kukidhi mahitaji ya wananchi wa Tanzania na kutokana na barabara zetu nyingi siyo imara hivyo hili gari litamudu katika majira yote yawe ya mvua au kiangazi” alimesa Minja.

Minja aliwahimiza Watanzania kutumia gari hilo kwa kuwa dhamani yake na uimara wake vinaendana na matumizi yake ya mafuta ni mazuri kulinganisha magari mengine aina hiyo kutoka kampuni zingine za magari. Alliance Autos Tanzania Ltd ni kampuni dada na kampuni ya CFAO Motors ya jijini Dar es Salaam.

Kampuni ya Arusha Art Limited ya jijini Arusha ambayo ni kampuni ya kuuza magari aina Mercedes-Benz, Nissan na Suzuki ndiyo itakuwa wakala wa kuuza gari hilo aina Volkswagen Amarok pickup katika mikoa ya kanda ya Kaskazini.


EmoticonEmoticon