JERRY MURO KUANZA KUPIGA KAZI LEO SAA 3 NA NUSU USIKU TBC


Napenda kuwajulisha wanamabadiliko kuwa kuanzia jumapili tarehe 10 mwezi huu,saa tatu na nusu usiku nitaanza kurusha mfululizo wa vipindi vyangu TBC.
 
Lengo la vipindi hivi ni kuonyesha kazi mbalimbali zilizofanywa na serikali kwa kushirikiana na taasisi ya mkapa foundation haswa katika masuala ya afya.
 
Vipindi pia vitaonyesha changamoto mbalimbali tunazokabiliana nazo katika sekta ya afya ili kwa pamoja tuweze kuzitatua haswa katika maeneo ya pembezoni mwa nchi(vijijini).
 
Vipindi hivi nimefanya mwenyewe na kampuni binafsi na vitarushwa TBC kwa ufadhili wa mkapa foundation.
 
Napenda ieleweke,mimi jerry muro sijaajiriwa TBC bali narusha vipindi vyangu pale kwa muda wa miezi miwili na nusu.
 
Mashabiki na wapenzi wa kazi zangu karibu tutazame ili pamoja tuweze kukabiliana na changamoto zinazolikumba taifa letu na hatimae tuweze kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.


EmoticonEmoticon