Baada ya kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa Tanzania bara na
mwakilishi pekee wa Afrika mashariki na kati katika michuano ya kimataifa,Wekundu
wa Msimbazi Simba na kuifanyia mauaji ya
kutisha Watani wao wa jadi Yanga ambayo ni klabu bingwa ya Afrika mashariki na
kati kwa kuifunga jumla ya goli 5-0,Wazee wa klabu ya Yanga wakiongozwa na
Akilimali Ibrahimu, umeweka wazi kilichopelekea timu yao kupokea kipigo kutoka
kwa Watani wao wa jadi.
Mzee Akilimali amesema timu ya Yanga iliingia kambini siku tatu kabla ya mchezo dhidi ya Simba huku wachezaji wakiwa hawana morali yoyote kutokana na kuwa walikuwa wakidai malimbikizo ya mishahara na bonasi za mechi za msimu mzima wa ligi kuu ya Vodacom.
Akilimali ameendelea kusema kuwa kwa muda mrefu kocha mkuu wa Yanga amekuwa akidai uongozi shilingi milioni 24 za malimbikizo ya mshahara wake, hali iliyopelekea Papic kutokuweza kuishi vizuri hivyo kupelekea kutokuwa na maelewano mazuri na uongozi.
Mzee Akilimali amesema timu ya Yanga iliingia kambini siku tatu kabla ya mchezo dhidi ya Simba huku wachezaji wakiwa hawana morali yoyote kutokana na kuwa walikuwa wakidai malimbikizo ya mishahara na bonasi za mechi za msimu mzima wa ligi kuu ya Vodacom.
Akilimali ameendelea kusema kuwa kwa muda mrefu kocha mkuu wa Yanga amekuwa akidai uongozi shilingi milioni 24 za malimbikizo ya mshahara wake, hali iliyopelekea Papic kutokuweza kuishi vizuri hivyo kupelekea kutokuwa na maelewano mazuri na uongozi.
Pia mzee Akilimali amesema madai ya bonsai kwa wanandinga hao ya
shilingi 70,000 kwa kila mchezo umechangia timu kufungwa dhidi ya Simba,lakini
katika hali ya kushangaza ndani ya kipindi chote cha Ligi kuu ya Tanzania bara
uongozi wa Yanga ukiongozwa na Nchunga haukuwalipa wachezaji bonasi za mechi
zote za msimu kama walivyokubaliana.
Akilimali amesema hali ya
kambi ilikuwa hairidhishi kifedha na kuwafanya wachezaji kutokuwa katika hali nzuri ya kiakili kuweza
kupambana na watani wao wa jadi na kuambulia kipigo kama kile mbele ya
mashabiki wao.
EmoticonEmoticon