Ngorongoro Heroes kuikabili Sudan leo jumamosi kuanzia majira ya saa mbili
usiku kwa saa za Afrika Mashariki ambayo itachezwa kwenye uwanja wa Khartoum
Sudan.
katika michuano ya Afrika kwa vijana
wenye umri wa miaka 20.
Mechi hiyo ya marudio ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri wa miaka
20 ambayo kwa mechi ya awali Ngorongoro Heroes iliikuba na ushindi wa goli 3
kwa 1.
Akizungumzia maandalizi ya mechi hiyo Afisa habari wa TFF Boniface Wambura
ambaye yupo na timu Khartoum amesema
kikosi kinafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Omdurman kiko katika hali nzuri na
kitatumia mfumo wa 4-4-2 kwa mujibu wa kocha wa kikosi hicho Kim Poulsen na
amesema nia ya kutumia mfumo huo ni kwa lengo la kushambulia muda wote wa
mchezo.
Wambura ameendelea kusema nyumbani tuliwafunga mabao 3-1, hivyo hapa
watacheza kwa kushambulia tu huku na sisi tukizuia mashambulizi yao kwa
kushambulia.
Kikosi cha Ngorongoro Heroes kinaundwa na; Aishi Manula, Jamal Mroki, Issa
Rashid, Samir Ruhava, Dizana Ramadhan,Frank Damayo, Frank Sekule, Omega Seme, Thomas
Ulimwengu, Simon Msuva na Ramadhan Singano.
Wachezaji wa akiba ni Saleh Malande, Hassan Dilunga, Ramadhan Khamis, Said
Zege, Jerome Lambele,
Emily Mugeta na Atupele Green.
Mtanange huo hautakuwa na kiingilio kwa washabiki watakao hudhuria
itachezeshwa na Aden Abdi Djamal wa Djibouti,akisaidiana na Wadjibouti wenzake
Egueh Yacin Hassan, Bogoreh Salime Fahan na Aden Ali Farah kamishna wa mchezo
huo ni Patrick Naggi wa Kenya.
Ngorongoro Heroes itaanza safari ya kurejea nyumbani mara baada ya mechi
hiyo, Itaondoka Khartoum saa 9 alfajiri kupitia Nairobi Kenya na kuwasili Dar
es Salaam Jumapili saa 3.20 asubuhi.
EmoticonEmoticon