SUNRISE RADIO YAPEWA TUZO YA HESHIMA NA AZAM FC

Dionis Moyo-Mkurugenzi Sunrise Radio

Kituo cha radio jijini Arusha cha Sunrise Radio kimepewa tuzo ya kituo bora kwa mkoa wa Arusha na klabu ya Azam fc kwa ushirikiano walioonyesha kwenye ligi kuu ya Vodacom iliyomalizika juzi huku Simba wakiibuka mabingwa wa ligi hiyo ya Vodacom.


Akizungumza kwa njia ya simu na Ezra Agora wa Sunrise Radio, Afisa habari wa Azam fc,Jaffari Iddi Maganga,amesema tuzo hiyo ya heshima wameitoa kwa Sunrise Radio Arusha kwa ushirikiano walioonyesha kwa Azam fc tangu mwanzo wa ligi kwa kuuliza kila kitu kinachoendelea klabuni hapo.


Ikiwa hiyo ni tuzo ya pili ya michezo Sunrise Radio wanapewa tangu mwaka huu uanze baada ya ile waliyopewa na Chama cha soka Manispaa ya Arusha mjini kwa kutangaza ligi ya Wilaya hiyo na pia wakitoa tuzo zingine kwa wanamichezo wa radio hiyo ambao ni Ally Shemdoe ambaye ni mhariri wa michezo wa Sunrise Radio na tuzo nyingine ilienda kwa Dionis Moyo ambaye ni Mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho.


Kwa upande wa Mhariri wa Michezo wa Sunrise Radio Ally Shemdoe amesema kwamba wameipokea tuzo hiyo ya heshima waliyopewa na Azam fc kwani ni kazi kubwa wameifanya kwenye mizunguko yote ya ligi kuu ya Vodacom.Pia amesema siyo Azam pekee ndiyo walikuwa wanaifuatilia bali timu zote zilizokuwa zinashiriki ligi kuu lakini Azam fc wameona mchango wao ndiyo maana wametoa tuzo hiyo ya heshima kwa Sunrise Radio.


Shemdoe ameendelea kusema kuwa wataendelea kutoa ushirikiano kwa timu zote hapa nchini lengo likiwa ni kukuza michezo Tanzania ili kufahamika kimataifa zaidi,pia ameviasa vyombo vingine vya habari kuonyesha ushirikiano ili kufanikisha na kuinua michezo Tanzania.


Hivyo Sunrise Radio imemteua muandaaji wa vipindi(Producer) Mussa Kinkaya kwenda jiji Dar siku ya Jumapili kwa ajili ya kuchukua tuzo hiyo ya heshima waliyopewa na Azam fc ambayo inatolewa simu ya Jumatatu kwenye ofisi za Azam jijini Dar.
Kwa upande wake Mussa Kinkaya amesema amefurahi Sunrise Radio kupewa tuzo hiyo ya heshima na Azam fc kama muandaaji wa vipindi kwenye kitengo hicho cha michezo.


Tuzo hizo zilitolewa na Azam fc siku ya Jumapili baada tu ya kumalizika kwa ligi kuu na Azam kushika nafasi ya pili hivyo kuamua kufanya sherehe ya kupongezana kwa mafanikio waliyoyapata kwa muda mfupi na kuahidi kufanya vizuri msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania.


Mbali na Sunrise Radio kupewa tuzo hiyo vyombo vingine vya habari vilivyopewa tuzo za heshima ni pamoja na TBC,Radio one na Mlimani zote za jijini Dar.


Kila la kheri Mussa Kinkaya kwa safari ya kwenda Dar kuchukua tuzo hiyo.


EmoticonEmoticon