AMKATA KATA MUMEWE KWA PANGA KISA PESA ZA MATUMIZI


Mwanamke mmoja  aitwaye Nuru mkazi wa Kwa  Mrefu mkoani Arusha anatuhumiwa kumkata vibaya kwa panga mume wake Edward John.

Tukio hilo limetokea jana huku mashuhuda wakidai kuwa amefanya hivyo kumshinikiza mume huyo kuacha tabia ya kutompa pesa za matumizi.

Taarifa za tukio hilo zinasema kuwa jana majira ya saa nne usiku, wakati majirani waliposikia kelele za kuomba msaada hivyo kuingia katika nyumba hiyo na kumkuta bwana huyo akiwa ameloa damu.

Hali ya Edward John bado ni mbaya, ingawa anaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru.


EmoticonEmoticon