NASARI ASAKWA NA POLISI BAADA YA KUMCHIMBA MKWARA KIKWETE ASIKANYAGE ARUMERU




Joshua Nasari-Mbunge Arumeru Mashariki

JESHI  la Polisi limempa masaa machache Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki Bw Joshua Nassari na endapo kama hatajisalimisha kwa jeshi hilo basi nguvu  zaidi zitatumika katika kumsaka kwa kuwa Mbunge huyo ametoa lugha za uchochezi kwa wananchi katika mkutano uliofanyika viwanja vya NMC ambao ulihudhuriwa na viongozi wa juu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA).

Akiongea na waandishi wa habariNaibu Kamishna wa jeshi la Polisi hapa nchini Bw Isaya Mngulu  amesema kuwa Mbunge huyo alitoa matamko hayo katika viwanja vya NMC ambapo alidai kuwa Rais hapaswi kufika katika kanda ya kaskazini hasa katika jimbo hilo endapo kama atashindwa kufuatilia sakata la mauaji  ya aliyekuwa kada wa  Chadema kwa haraka sana

Aidha Mngulu aliongeza kuwa  mbali na mbunge huyo kusema maneno hayo pia aliwaambia wananchi waliokuwa katika maeneo ya viwanja vya NMC kuwa  yeye ndiye atakayekuwa Rais  wakati  Waziri mkuu atakuwa ni Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Bw Goodbless Lema hali ambayo inaonesha kauli za uchochezi.

Akiongelea sakata la baadhi ya wanachama wa Chadema kudai kuwa wanatishiwa kuuawa na watu wasiojulikana kuwa madai hayo ni ya uongo na wanaotuma na kusambaza ujumbe mfupi(SMS) ni  makada wa Chadema na mpaka sasa Jeshi hilo limeshawabaini.
Awali alisema kuwa mpaka sasa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanikiwa kuwatia Mbaroni watu12 ambao walihusika na Mauaji mbalimbali katika eneo la Meru ambapo watu 3 wameshafikishwa mahakamani huku wengine wakiwa wanaendelea na uchunguzi  katika  tukio la kuuawa vibaya kwa Kada wa Chadema wiki chache zilizopita.

Pia alisema kuwa mbali na kuweza kuwashikilia watu hao 12 ambao wanahusika na  mauaji ya Kada wa Chadema pia bado jeshi hilo linaendelea na upelelezi zaidi ili kuweza kuwatia mbaroni pia waliohusika na mauaji ya bibi kizee Bi Martha Joseph(77) kwa madai kuwa alikuwa ni mchawi katika eneo la Nkoaranga


EmoticonEmoticon