LEO, Real Madrid wako Ugenini huko
Estadio Balaidos kucheza Mechi yao ya Kiporo na Celta Vigo na ushindi
kwao utawaweka Pointi 3 mbele ya Barca huku Mechi zikibaki 1 kwa kila
Timu.
La Liga itafikia tamati Jumapili Mei
21 na hadi sasa Barca na Real ziko juu kileleni zikifungana kwa Pointi
lakini Barca wanaongoza kwa Rekodi yao Bora ya uso kwa uso na Real.
Hata hivyo, Real wana Mechi 1
mkononi na ndio hiyo wanayocheza leo na wakishinda leo basi Jumapili
kwenye Mechi yao ya mwisho Ugenini na Malaga watahitaji Sare tu ili
watwae Ubingwa wao wa kwanza wa La Liga tangu 2012.
Hivi sasa Celta Vigo wapo Nafasi ya
13 kwenye La Liga na hawajashinda mechi tangu katikati ya Mwezi Aprili
wakifungwa Mechi 6 kati ya 7 walizocheza tangu wakati huo ambapo pia
walitupwa nje ya Nusu Fainali ya Europa League na Manchester United.
Licha ya takwimu hizo, Kocha wa
Real, Zinedine Zidane, amesisitiza mechi hii ni kama fainali kwao huku
akithibitisha kuwemo Kikosini mchezaji Bora Duniani Cristiano Ronaldo.
Nae Kocha wa Celta Vigo, Eduardo Berizzo, amesisitiza mechi hii ni nafasi safi kwao kufuta matokeo mabovu yao ya hivi karibuni.
Katika mechi ya Kwanza ya La Liga msimu huu iliyochezwa mwezi Agosti huko Santiago Bernabeu Jijini Madrid,
Real iliichapa Celta Vigo 2-1 kwa bao za Alvaro Morata na Toni Kroos
wakati lile la Celta lilifungwa na Fabian Orellana.
LA LIGA
Ratiba:
**Saa za Bongo
Jumatano Mei 17
22:00 Celta Vigo v Real Madrid
Raundi ya 38 – Mechi za Mwisho
Ijumaa Mei 19
21:45 Granada v Espanyol
Jumamosi Mei 20
18:00 Deportivo v Las Palmas
18:00 Sporting Gijon v Real Betis
18:00 Leganes v Alaves
Jumapili Mei 21
17:45 Atletico Madrid v Athletic Club
17:45 Celta Vigo v Real Sociedad
17:45 Sevilla v Osasuna
17:45 Valencia v Villarreal
21:00 Barcelona v Eibar
21:00 Malaga v Real Madrid
EmoticonEmoticon