UHAKIKI WALIMU KILIMANJARO KUWARUDISHA NYUMA KIUCHUMI


CHAMA cha walimu (Cwt) Mkoa Wa Kilimanjaro kimebainisha mapungufu
katika zoezi la uhakiki wa walimu,kutokana na zoezi hilo kuchukua
muda mrefu na gharama kubwa ya usafiri  ambazo  ni sehemu za
mishahara yao.

Akizungumza na mwandishi wa habari mjini Moshi Mkoani humo  katibu wa
chama cha walimu (Cwt)mkoa Kilimanjaro,Ally  Mbaga amesema kuwa zoezi
hilo limekuwa  na mapungu mengi kutokana na kuchukua muda mrefu huko
wanafunzi wakikosa vipindi vingi.

Amesema kuwa    zoezi  la uhakiki wa walimu limekuwa la  mateso kutokana
na walimu  kutumia wiki mbili hadi tatu kwa ajili uhakiki ambapo
wanatumia gharama kubwa za usafiri na malazi kwa walimu wanaoishi
sehemu za vijijini  ambazo fedha hizo  ni sehemu ya mishahara yao.

Amesema maeneo mengi katika mkoa wa Kilimanjaro  hadi kufika vituo vya
uhakiki wanalazika kutumia zaidi ya sh.40000 hadi 50000  na ni
vema sasa serikali ikaangalia namna nyingine ya kufanya uhakiki kwa
kuwafuata kwenye vituo vyao vya kazi ili kuondoa adha hiyo.

Mbaga aliendelea kueleza kuwa tatizo la ucheleweshwaji malipo ya walimu
waliopandishwa madaraja katika mkoa Kilimanjaro bado ni changamoto
kwa walimu wengi waliopandishwa madaraja kwa muda mrefu hawajalipwa
hadi sasa.


EmoticonEmoticon