ZANZIBAR HEROES YASHIKA NAFASI YA TATU


Timu ya taifa ya Zanzibar 'Zanzibar Heroes' imerejea jana kutoka nchini Kurdistan wakiwa wameshika nafasi ya tatu katika michuano ya VIVA Wordcup iliyomalizika juni 9 mwaka huu.

Michuano hiyo ya dunia ilihusisha mataifa yasiyo wanachama wa shirikisho la mpira wa miguu la kimataifa 'FIFA' ambapo mataifa 9 yalishiriki mashindano hayo nchini Kurdistan.


Zanzibar Heroes wameshika nafasi hiyo baada ya kuwachalaza Province ya Ufaransa magoli 7-2 katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu uliochezwa juni 9.


Zanzibar Heroes walikwaana na Province baada ya kufungwa na Cyprus goli 2-0 katika mchezo wa nusu fainali.


Zanzibar Heroes walitinga hatua ya nusu fainali baada ya kushinda goli 6-1 kabla ya kushinda goli 3-0 na kufanikiwa kuingia hatua hiyo wakiwa vinara wa kundi B lililokuwa na timu 3.


Mshambuliaji wa Azam FC Khamis Mcha Viali aliibuka mfungaji bora wa michuano hiyo.


EmoticonEmoticon