SIMBA WAHITAJI BILIONI 2 KUMWACHIA OKWI



Mabingwa wa Tanzania wekundu wa Msimbazi Simba SC wametangaza bei ya mshambuliaji wao hatari na mfumania nyavu EMMANUEL OKWI kwa timu yoyote inayomtaka kwa kufuata masharti.

Akizungumza na SUNRISE RADIO mapema leo msemaji wa mabingwa hao,EZEKIEL  KAMAGWA amesema kuwa kwa timu yeyote ile inayomtaka mshambuliaji wao huyo wawe tayari kutenga kiasi cha shilingi EURO 850,000/= ambayo ni sawa na shilingi bilioni mbili za kitanzania.

KAMWAGA amesema wamepata ombi kutoka nchini AUSTRIA ya mawakala wanamlilia kutaka kumpeleka nchini humo kusakata kabumbu hivyo wamewaambia kama wanaweza kulipa BILIONI 2 za Kitanzania watamchukua OKWI.

Mawakala hao wamesema kwa sasa wanatafakari kumnunua mchezaji huyo kwani ana kiwango cha hali ya juu hasa katika kupachika mabao hivyo atawafaa katika timu yao na wanafikiria dau hilo waliloambiwa na Uongozi wa mabingwa hao.
Pia amesema kama klabu inamhitaji OKWI lazima ifuate masharti matatu ambayo ni MAISHA MAZURI KWA WACHEZAJI,MISHAHARA na UONGOZI BORA.

KAMAGWA amesma  timu za YANGA na AZAM zimeshindwa kufikia dau hilo na kuitaka YANGA kufanya uchaguzi ndo waje kuongea na Uongozi wa Simba kwani YANGA kwa sasa hawana uongozi hivyo kutokana na masharti hayo waliyoyataja.

KAMWAGA ameendelea kusema kuwa wameweka dau hilo kwa OKWI kwani ana uwezo mkubwa kisoka na angekuwa Ulaya thamani yake ingekuwa mara tatu au  nne kwa dau walilotoa hivi sasa.


EmoticonEmoticon