YANGA KUCHUKUA MILIONI 600 LEO ?

Kikosi cha Yanga tayari kimekamilisha maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Wolaita Dicha kuelekea mechi itakayopigwa leo mjini Awassa, Ethiopia.

Meneja wa timu, Hafidh Saleh, ameeleza kuwa tayari kikosi kimeshakamilisha mazoezi yake na wako tayari kwa mtanange huo.

Saleh amesema wachezaji wote wako fiti kucheza leo na
hakuna aliye majeruhi.


Yanga itasonga mbele kwenye mashindano hayo mpaka hatua ya makundi endapo itatoa sare yoyote ile ama kuibuka na ushindi.

Katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa Dar es Salaam, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Kusonga mbele kwa Yanga kutaiwezesha kutwaa zaidi ya milioni 600 za kitanzania kama ilivyo utaratibu wa CAF kutoka kitita hicho cha pesa.

Latest


EmoticonEmoticon