CELTA VIGO YAIBANIA FC BARCELONA NJE NDANI LA LIGA

Barcelona imeendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa ligi kwa kuwa na alama zake 83 kati ya michezo 33 iliyocheza.
Barcelona ililazimisha sare ya mabao 2-2 ikiwa ugenini katika Ligi Kuu Spain,huku mabao yake yakifungwa na Dembele dakika ya 36 na la pili likitiwa kimiani na Alcacer mnamo dakika ya 64.
Kikosi hicho kilicheza kikiwa pungufu kuanzia dakika ya 71 baada ya Sergi Roberto kulimwa kadi nyekundu.
Celta Vigo imekuwa timu pekee ambayo imeshindwa kupoteza mbele ya Barcelona msimu huu baada ya kuilazimisha Barcelona kupata matokeo ya sare katika michezo yote miwili ya ligi.
Hiyo imekuwa ni rekodi kwa Celta ukiangalia baadhi ya vigogo wengine kama Atletico na Real Madrid tayari wameshapokea vichapo kutoka kwa vinara hao wa ligi msimu huu.


EmoticonEmoticon