BOCCO ATAMBULISHWA RASMI SIMBA

SIMBA SC imemtambulisha mshambuliaji wake mpya, John Raphael Bocco ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na Wekundu hao wa Msimbazi akitokea Azam FC.
Rais wa Simba SC, Evans Elieza Aveva leo amemkabdhi jezi ya klabu hiyo nahodha wa zamani wa Azam FC, kufutaia kukamilisha taratibu za kujiunga na timu hiyo kongwe nchini.
Bocco, kama wachezaji wengine wa Azam wanaokwenda Simba, kipa Aishi Manula na beki Shomary Kapombe inafuatia kutofikia makubaliano ya kuongeza mikataba Azam FC.


EmoticonEmoticon