SIMBA SC YAIUNGA MKONO SERIKALI KUHAMIA DODOMA


Klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba leo August 30 2016 kupitia kwa mkuu wake wa idara ya habari na mawasiliano wa klabu hiyo Haji Manara imetangaza kuwa itacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Polisi Dodoma.

Simba itacheza mchezo huo wa kirafiki siku ya Jumamosi ya September 3 2016 katika uwanja wa Jamhuri Dodoma kama sehemu ya kuunga mkono wazo la serikali kuhamishia makao makuu Dodoma.

“Tutacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Polisi Dodoma siku ya Jumamosi ya September 3 kuunga mkono wazo la Rais Magufuli kuhamishia serikali Dodoma, tutaondoka hapa siku ya Alhamis kuelekea Dodoma lakini tutakuwa na bango ambalo litashikwa na wachezaji likionesha kuunga mkono kwa wazo hilo”


EmoticonEmoticon