![]() |
Yusuf Manji |
Baada ya kuapishwa, viongozi wa Yanga walifanya kikao cha
Kamati ya Utendaji, ambacho kilifikia uamuzi wa kuvunja Kamati zote ndogondogo
ili kuunda Kamati mpya.
Mwenyekiti wa Yanga, Yussuf Manji alisema Kamati ambayo
haitaguswa ni Kamati ya Uchaguzi pekee, iliyo chini ya Mwenyekiti Jaji John
Mkwawa.
Baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji, Manji alifanya kikao
kingine kidogo na wanachama, akiwa na Makamu wake, Clement Sanga.
Kutoka hapo,
Katibu wa Yanga, Celestine Mwesigwa akaenda kuzungumza na Waandishi wa Habari,
kuwapa yaliyofikiwa kwenye Kamati ya Utendaji.
Alikosekana Abdallah Bin Kleb pekee, ambaye yupo Kigali, Rwanda kwa majukumu ya klabu.
EmoticonEmoticon