TFF WAGOMA KUMLIPA MSHAHARA HEWA KOCHA POULSEN


SHIRIKISHO la Soka Tanzania(TFF) limeweka wazi kwamba aliyekuwa kocha wa timu ya taifa(Taifa Stars)Mdenmark Jan Poulsen hatalipwa mishahara yake ya miezi mitatu iliyosalia katika mkataba wake.

Msimamo huo wa TFF umekuja wiki iliyopita bada ya Poulsen kulilalamikia shirikisho hilo kwa kutomlipa mshahara wake wa mwezi mmoja,sambamba na fidia inayotokana na kuvunjwa kwa mkataba wake.
Hivi karibuni TFF ilisitisha huduma ya Poulsen kwa Taifa Stars na badala yake ikamtangaza aliyekuwa kocha wa timu za taifa za vijana, Kim Poulsen kuchukua jukumu hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema kuwa hatua ya kutomlipa Poulsen mishahara ya miezi mitatu inatokana ukweli kwamba kocha huyo hatakuwa na kazi ya kufanya katika kipindi hicho cha miezi mitatu ya mkataba wake kilichosalia hadi Julai 30.

"Kwanza kabisa ieleweke kwamba kwamba serikali ndiyo iliyokuwa inamlipa  Poulsen mshahara baada ya kuingia naye mkataba na sio TFF."Katika utaratibu wa kawaida wa serikali tunaoufahamu awezi kulipwa mshahara wa bure wakati hajafanya kazi yoyote,huo ndio ukwli wenyewe,"alisema Wambura

Akifafanua zaidi, Wambura alisema TFF iliamua kusitisha huduma za Poulsen licha ya kwamba mkataba wake unaendelea kuwa hai kwa lengo la kutoa nafasi kwa kocha mpya kupanga mipango ya muda mrefu.

"Kila baada ya muda fulani kocha anatakiwa awasilishe ripoti ya timu yake,sasa utapataje ripoti sahihi wakati kesho kutwa mkataba wake unamalizika.

"Pia niweke vizuri hapo,TFF haikuvunja mkataba wa Poulsen bado upo na utamalizika Julai 30 tulichokifanya ni kuzungumza nae na kukubaliana kwamba hakutaongeza mkataba hivyo tunatafuta kocha mwingine,"alisema.

Wambura aliongeza kuwa,licha ya kibarua cha kocha huyo cha kuinoa Taifa Stars kusitishwa,bado TFF itaendelea kuwa nae katika mkataba mwingine unaohusiana na ukufunzi wa makocha nchini.

"Poulsen pia alikuwa na kazi nyingine ya ukufunzi wa makocha hata hapa ametuaga anakwenda kwao kuhudhuria harusi ya mtoto wake akirudi ataendelea,"alisema Wambura

Kwa  upande mwingine kusitishwa kwa kibarua cha Poulsen kunahusishwa  na shinikizo la wadau wa soka waliotaka mabadiliko katika benchi la ufundi kufuatia Taifa Stars  kuporomoka mfululizo kwa takribani miezi saba kwenye viwango vya ubora vya Shiriki


EmoticonEmoticon